Wednesday, December 17, 2008

ARI-SELIAN nawapa shavu kwa usafi

Nipo Arusha kikazi pamoja na watafiti wa hapa. Kilichonileta hapa ni kuwasilisha miongozo na kujadiliana na watafiti waandamizi jinsi ya kuandaa viashiria vya shughuli za utafiti kanda ya kaskazini. Lakini kilichonivutia zaidi wakati nikiwa hapa kituoni Selian ni usafi wa mazingira hasa vyoo. Vyoo ni visafi kweli kweli sabuni zipo na watumiaji ni wastaarabu kwa kweli.

Tabia ya usafi katika kituo cha Utafiti wa Kilimo Selian imejengwa kwa muda mrefu kwa sasa ni utamaduni uliozooeleka hapo kituoni watakushangaa kama unachafua mazingira yao bila sababu. Hongera sana Selian.

No comments: