Monday, December 29, 2008

Dakika 120 Matombo-Moro

Nimerudi kutoka Matombo. Mambo yalikuwa safi sana huko kijijini. Nimekula magimbi, mananasi, maembe na ubwabwa. Lakini cha kushangaza mwaka huu kuku ni wachache sana Matombo. Hata wa kununua hawapatikani. Kuku imekuwa ni dili kubwa sana Matombo. Unawaona lakini hauwzwi!

Ndiyo, barabara ya Matombo kwa sasa ni nzuri mno! Ndiyo maana tumeweza kutumia dakika 120 kufika Matombo kutoka Morogoro mjini kwa kutumia kibus cha 'Hiace.' Msalabani hadi Matombo Mission barabara imenyanyuliwa hata corolla inapita! Ni kweli walionazo walikuja nazo kushrehekea Xmass kijijini. Pale Chamarigo (Gubi) ambapo huwa panasumbua sana wakati wa mvua sasa pamewekewa Culvert. Safi sana. Hongera Tanroads, Hongera Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Vijijini.

No comments: