Friday, December 5, 2008

Vijana wakiafrika sasa hufanya biashara nchi mbalimbali

Kuchelewa kuondoka uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyata siku ya tarehe 26 Novemba 2008 kumenifanya nijifunze mengi.

Wakati nilipokuwa napata chakula cha mchana cha kuponi pale uwanjani (kutokana na kucheleweshwa) niliwaona vijana wengi wake kwa waume. Nilibahatika kumuuliza mmoja wao anatokea wapi alinijibu anatoka Nigeria na anelekea Bangkok kwa shughuli ya biashara. Kwenye meza nilizunguukwa na vijana wanne waliokuwa wakizungumza kifaransa nao wako kwenye pilika ya safari za kibiashara. Nilishindwa kudodosa zaidi nijue ni biashara ya aina gani wanayofuata huko Bangkok. Sote tulikuwa tunasubiri chakula!

No comments: