Wednesday, December 31, 2008

Amri inapotolewa kupumzisha MV Magogoni

Ijumaa ya tarehe 19/12/2008 saa 2.30 usiku nilipitia Kivukoni ili niweze kurudi Nyumbani kwangu Kisemvule kwa kuogopa adha ya usafiri kupitia njia ya Mbagala huku nikitegemea kuwa kwa sasa usafiri wa boti umeimarika zaidi baada ya boti MV Magogoni kuzinduliwa mwanzoni mwa mwezi Desemba mwaka huu.

Cha kushangaza mara boti hilo MV Magogoni lilipotia nanga likitokea Kigamboni Captain aliamrishwa na bosi wake akiwa nyumbani kuwa asimamishe boti hilo na boti za zamani zitumike.

Hali hii iliwakera sana abiria kiasi cha kumzonga Captain.
Sidhani kuwa ilikuwa na mantiki kusimamisha boti hilo kwa wakati huo tena kwa amri kutoka nje ya sehemu ya kazi! Tulikuwa na matatizo ya boti usafiri taabu. Boti jipya limeletwa usafiri ni taabu. Hivi Watanzania tuna nini?

No comments: