Tuesday, December 30, 2008

Mitandao ya simu Matombo hajaisaidia sana maisha ya wakulima

Miaka miwili tangu Kampuni ya simu ya Celtel (sasa Zain) iingie Matombo, ushindani wa mitandao ya simu umeongezeka kwa kasi ya kutisha Matombo. Tigo wakasimika mnara wao kwenye mlima wa "Funamandole" mwaka jana na kuufanya mtandao huo kuwa bora zaidi ya Celtel.

Mwaka huu Vodacom imeingia Matombo na kufunika kabisa Zain na Tigo. Lakini sidhani ushindani huu unawasaidia sana wakulima masikini wa Matombo kwani mawasiliano ya simu za mkononi bado ni ghali mno hasa mawasiliano yakifanyika kwa mitandao tofauti. Hili linabidi kufanyiwa kazi na vyombo husika ili wakulima hao wasiwe wanapoteza fedha nyingi zaidi kwa mawasiliano kuliko chakula!

No comments: