Friday, December 5, 2008

Ulemavu si hoja

Niko Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Jomo Kenyatta nikisubiri ndege yakunirudisha nyumbani Dar. Jirani yangu yuko mama mmoja wa kizungu (baadaye nakajakugundua kuwa ni Mswede) yuko "busy" na laptop yake na kifaa kingine (sikijui). Nashangaa nagundua kuwa ni kipofu lakini ana jamaa zake wawili alioandamana nao.

Baadaye nagundua kuwa naye anasafiri kuelekea Tanzania tena Morogoro. Nilifahamu hivyo baada ya kusikia mazungumzo yao na yule Mmasai kutoka Twatwatwa, Kilosa na mama mmoja kutoka Sudan. Mama huyu licha ya kutoona alikuwa na vifaa vya kisasa vinavyomsaidia kuendesha shughuli zake kama vile kutumia kompyuta. Na wakati akizungumza huwezi kugundua kama ni kipofu, ufahamu wake ulikuwa ni wa hali ya juu. Ama kweli Ulemavu si hoja.

No comments: