Wednesday, December 31, 2008

Lami yaanza kumwaga Kilwa Road

Wakati tunasherehekea kuingia kwa mwaka mpya, wakazi wa Mbagala na vitongoji vyake wameanza kuonja raha ya usafiri baada ya kupungua kwa foleni za magari katika barabara hiyo hasa kutoka Mtoni Mtongani hadi Sabasaba.
yapata wiki ya pili sasa kipande cha barabara hiyo kinachoanzia Mbagala Rangi 3 hadi karibu na Kizuiani kimeshawekwa lami kwa upande mmoja. Uwekaji wa lami unakaribia kabisa eneo la sabasaba (St. Anthony Sec.School).

Yale madaraja mawili ya mtoni Kizinga wamekamilika kwa asilimia 94. Ni matumaini yangu kuwa ifikapo mwezi Aprili 2009. Wakazi wa Mbagala watakuwa wanateleza kwenye Highway. Tatizo la usafiri Mbagala litakuwa historia.

No comments: