Friday, January 2, 2009

Mwaka mpya Tulikuwa kwa Luanda

Kwangu mimi mwaka 2009 uliingia bila papara. Sikuweza kungojea hadi saa sita usiku eti nipige madebe au vibweka au kugongeana glass za vinywaji. Natumaini wakati ndo unasogea, makeke yamepungua. Ilipofika mwaka 2009 tayari nilishachoka na kujitupa kitandani.

Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunilinda kuwa hai hadi kufikia tarehe ya leo. Mengi yametokea mwaka 2008 ambayo yangeweza kupoteza uhai wangu. Magonjwa ajali na mengineyo.

Hata hivyo lazima niseme kuwa ubinadamu ni pamoja na kuwa na watu. Mimi na familia yangu tulikaribishwa kule Kigogo darajani nyumbani kwa ndugu yangu na rafiki wa siku nyingi ambaye tumesoma wote shule ya msingi na hatimaye sekondari ya Njombe Bw. Michael Luanda.

Kwa miaka kadhaa sasa Michael hakuwa hapa jijini ila familia yake ilikuwa hapa. Sasa Michael amerudi tena Dar. Tarehe 1/1/2009 tuliitumia kwa kula, kunywa kidogo, gumzo pamoja na kujadili mambo mengi yaliyopita na si ya mwaka 2008 tu bali yote ambayo tuliweza kuyakumbuka.

Tunaishukuru sana Familia ya Michael Luanda kwa kutukaribisha kusherehekea pamoja Mwaka mpya 2009.

No comments: