Tuesday, January 27, 2009

Tulitembea na kutembea

Mvua ya jana imeleta kizazaa kwa wakazi wa Mbagala na vitongoji vyake. Kutokana na msongamano wa magari na magari mengine kukwama kwenye barabara mpya inayojengwa usafiri ulikuwa wa shida sana siku ya jana jioni hadi leo asubhi.

Blog hii ilichapa mguu kutoka Mtoni Mtongani hadi KTM. Leo asubuhi Mbagala Rangi 3 kulikuwa hakuna mabus. Blog hii iliweza kulipa shilingi elfu 1000 kutoka Rangi 3 hadi Kizinga na kuanza kutembea tena hadi Mtoni Mtongani.

Lakini matatizo haya si kutokana na ujenzi wa barabara bali ni ubinafsi wa madereva kutaka kuwahi bila kujali wengine. Pia askari wa usalama wa barabarani nao wanazembea. Matokeo yake gari zinafungana.

No comments: