Wednesday, January 14, 2009

Ukaguzi wa mabasi asubuhi si suluhisho la ajali

Watu wanazidi kufa kwa ajali za kutisha barabarani. Ajali ya hivi karibuni iliyohusisha basi la Tashrif na kupoteza uhai wa watu karibuni 28 si kitu cha mchezo ni tatizo.

Kinachonishangaza ni kwamba tatizo hilo ni la muda mrefu na ufumbuzi wa tatizo hili bado sijaliona. Sababu kubwa inafahamika ni uendeshaji usio na tahadhari. Blog hii imeshasafiri sehemu mablimbali kwa kutumia mabus ya kampuni mbalimbali. Ilichoshuhudia ni uendeshaji usio wa tahadhari. Lakini cha ajabu abiria hushabikia mwendo wa kasi bila sababu ya msingi. Alama za barabarani zipo lakini hakuna dereva anayejali.Wao wanapeana taarifa kwa traffic walioko barabarani basi. Nafikiri adhabu zinazotolewa bado ni ndogo na hazitoi fundisho lolote. Labda niwe mkweli tu hata dereva anapovunja sheria anawahonga matrafiki mambo yanakwisha. Blog hii ilishakutwa na tukio hilo nikiwa kwenye safari ya kikazi kuelekea Arusha tena na gari la serikali tulikuwa tukisafiri km 60 kwa saa wakati sehemu hiyo tulitakiwa kuendesha 50 km kwa saa. Trafki alituzungusha akitaka tumpe kitu kidogo. Sisi tulisema hatuna!

Magari makubwa nayo ni moja ya chanzo cha ajali nyingi barabarani. Yakiwa njiani hufanya lolote. Hupaki hovyo wanapoona wao. Tena pengine kwa sababu ya kipuuzi kabisa (kwa nyumba ndogo!) haaweki alama yoyote. Usiku mzima gari limeegeshwa vibaya! Madereva wanaendekeza ulevi wakati wanajua kuwa wako barabarani.

Blog hii inasema kuchek magari asubuhi ni kero kwa abiria na wamiliki wa magari. Magari yakaguliwe wakati yanaingia kituoni kabla ya safari ya kesho. Kwa yale yanayofanya usafiri wa umbali mfupi kama vile Dar-Moro utaratibu mwingine utumike. Ajali hutokea huko barabarabi si vituoni.

No comments: