Thursday, January 22, 2009

Hata mimi sikutegemea kama Obama angekuwa Rais wa Marekani

Kwa watu walio wengi si rahisi kusema ukweli wao walivyofikiri kabla ya tukio kutokea na kuwa kinyume chake. Lakini Bi.Mwakitwange waliokuwa pamoja na Tido Mhando katika TBC1 (TV) wakirusha matangazo ya mojakwamoja wakati wakuapishwa Rais mpya wa Marekani -Rais Barack Hussein Obama alisema kuwa kwa jinsi anavyoifahamu Marekani na hasa watu weupe hakutegemea kuwa Obama angepata kura za kutosha kumfikisha "White House." Tuseme ukweli si rahisi sana kwa mzungu kumwamini mweusi kuwa naye anaweza tena katika ngazi kubwa kama ile. Hata mimi sikutegemea kama Obama angeweza kuingia White House kwa sababu weupe nawafahamu sana wengi wanatuona hatuwezi! Hongera sana Obama na Familia yako. Hongera waamerika kwa kufanya kile ambacho hapo awali wengi wetu tulifikiri hakiwezekani.

No comments: