Saturday, January 24, 2009

Tujaribu usikate tamaa

Tatizo kubwa ninaloliona mimi kwa Watanzania wengi ni kukata tamaa katika maisha yetu. Wanafunzi wanakata tamaa kuwa hawawezi kufaulu hesabu na kiingereza. Wakulima wanakata tamaa kuwa mazao wanayolima hayana bei kwahiyo wanalima kidogo tu. Dereva wa daladala haondoi gari mapema kituoni kwani anakata tamaa kuwa hakuna abiria wengine kituo kinachofuata. Mchezaji mpira wa timu ya Taifa anakata tamaa kuwa hawawezi kuishinda Ivory Coast!

Tunjaribu tena na tena tusikate tamaa iko siku tutafanikiwa tukijatihidi na kuweka malengo.

No comments: