Saturday, January 24, 2009

Tupunguze kuomba misaada isiyo ya lazima

Ukipanda daladala utasikia konda msaada hapo kwenye kona! Unapokuwa ofisini mnahimizwa kuandika maandiko ya miradi ya maendeleo ili muweze kupata msaada kutoka kwa wafadhili.
Unarudi nyumbani jirani yako anakuomba msaada wa chumvi!
Mtoto wa ndugu yako anataka kuoa msaada!

Kuna misaada tunayoomba ambayo ni muhimu kama vile ya elimu, afya au msiba. Lakini mingine si muhimu sana.Ikiwezekana tusimame wenyewe kama mtu binfasi au kama nchi. Na tabia hii ya abiria kuomba msaada hata kwenye mlima au kona ili ateremshwe ikome inasababisha ajali na si ustaarabu. Tuheshimu vituo vilivyowekwa.

No comments: