Saturday, January 24, 2009

Kweli tununue matrekta na siyo mashangingi

Rais Jakaya Mrisho Kikwete ameahidi kuwa serikali itabana matumizi ya ununuzi wa magari ili fedha hizo zipelekwe kununulia matrekta kwa ajili ya wakulima. Nafikiri sasa kinaeleweka kwa wakulima - twendeni tukalime.

Waziri Mkuu ameahidi kuongeza bajeti. Rais naye ameahidi matrekta yanunuliwe badala ya magari. Ndiyo, sasa tumepata viongozi watetezi wa wakulima. Tuchape kazi uzalishaji katika sekta ya kilimo uongezeke na uchumi wa nchi ukue na wananchi waishi maisha bora.

No comments: