Monday, January 26, 2009

Hapa ni pabaya

Watanzania wenzangu, hapa tulipofikia sasa ni pabaya. Iwapo tunaamini kuwa tunaweza kupata maendeleo kwa njia ya ushirikina basi tumekwisha. Watoto hawatasoma, wafanyakazi hawatofanyakazi kwa bidii. Wakulima watalaza majembe yao chini.

Kisa? Mbona unaweza kutajirika kwa kuwa na mkono wa zelu zelu(Albino)! Unaweza kufaulu mtihani wa darasa la saba kwa kidole cha zelu zelu. Unaweza ukapata madini ya Tanzanite hivi hivi tena bila kuyaona wala kuchimba ikiwa utakuwa na kiganja cha zelu zelu na unaweza kwenda Marekani ikiwa utakuwa na korodani ya zelu zelu - STUPID!

No comments: