Thursday, January 22, 2009

Kilimanjaro Stars ilikuwa na nafasi nzuri ya kutwaa kombe la "Challenge"

Nachukua fursa hii ya kuipongeza Timu yetu ya Mpira wa miguu ya Tanzania Bara - Kilimanjaro Stars kwa kushika nafasi ya tatu ya mashindano ya Challenge cup yalifanyika nchini Uganda jijini Kampala mwaka huu.

Hata hivyo, kwa mtazamo wangu Kilimanjaro Stars ilikuwa na nafasi nzuri ya kushinda kombe hilo kutokana na jinsi walivyojitayarisha na kujengewa uwezo wa kila hali.

Stars ilikuwa na wachezaji wengi wazuri ambao juzi juzi tu wameweza kuifanikisha Taifa Stars (wachezaji wa ndani) kupata fursa kuingia kwenye fainali za mashindano ya ubingwa wa Afrika kwa wachezaji wasio wa kulipwa.

Tatizo kubwa kwa watanzania ni kutojiamini na kujituma kwa kila hali. Hii si kwa mchezo wa mpira peke yake hata katika shughuli nyingine. Hivyo basi ili tuweze kushinda siku zijazo timu itayarishwe vizuri kisaikolojia. Mpira tunaujua ila tunakosa mbinu basi tuwe na jopo litakalosaidia kutoa mbinu au mikakati ya ushindi.

No comments: