Monday, January 26, 2009

Nimefurahishwa wakulima kugawa vyandarua

Gazeti la Majira la tarehe 19/01/2009 lilikuwa na habari nzuri inayohusu wakulima wadogo wa chai wilayani Rungwe (RSTGA) kugawa vyandarua 120 kwa akina mama wanaojifungua watoto kwa lengo la kupunguza kasi ya ugonjwa wa malaria.

Akina mama hawa wameonyesha njia. Kwanza wametambua tatizo na wamelifanyia kazi kwa sababu linawahusu zaidi wao na watoto. Kumbe hata sisi tunaweza kununua vyandarua hata kama ni vichache.

Viko wapi vyandarua vya Rais mstaafu wa Marekani Bw. George Bush? Au ndo tuseme ahadi hiyo haitekelezeki?

No comments: