Thursday, January 22, 2009

KILWA ROAD UPDATE 2!

Ukarabati wa barabara ya Kilwa, kipande cha Mtoni Mtongani hadi Mbagala Rangi 3 unaendelea vizuri. Tangu Jumapili 18 Januari madaraja ya mto Kizinga yameanza kutumika (siyo rasmi) hivyo kuondoa wasiwasi kwa watumiaji wa barabara hiyo -Masika itakuwaje? Uwekaji wa lami nao unaandelea kwa kasi nzuri tu. Tatizo lipo kidogo pale KTM - kwenye makutano ya barabara ya Kijichi na Kilwa kiasi cha kusababisha kafoleni kadogo hivi lakini si kama zamani. Umeshanunua kiwanja Mbagala? Karibu - unachelewa!

No comments: