Wednesday, January 14, 2009

KILWA ROAD UPDATE!

Ha! barabara ya Kilwa kipande cha Mtoni Mtongani hadi Mbagala Rangi 3 ndo kinakaribia kumalizika. Blog hii imeamua kuwapatia maendeleo ya ukamilishaji wa kipande hiki kila inapobidi. Hii inatokana na ukweli kuwa kwa miaka mingi Mbagala imeonekana kuwa na tatizo sugu la usafiri kutokana uchakavu wa barabara yake na ufinyu wa barabara hiyo ukilinganisha na magari mengi yanayotumia barabara hiyo. Hata kusababisha watu kuwakejeli watu wanaoishi Mbagala!

Kampuni ya Ujenzi ya Kajima inandelea vizuri sana. Madaraja mawili pale mtoni Kizinga yameshakamilika. Kilichobaki ni kushindilia udongo pamoja na mambo mengine madogo madogo-nakshi nakishi.

Huwezi kuamini barabara hiyo kwa sasa ni kama vile uwanja wa Taifa mpya kwani una nyavu kando ya barabara sehemu ambazo zimenyanyuliwa sana ili kuepusha magari na waendeo kwa miguu wasitumbukie korongoni.

Ukitoka Mbagala Rangi 3 upande wa kushoto tayari lami imeshawekwa hadi KTM. Baadhi ya sehemu magari yameshaanza kutumia kipande hicho kilichowekwa lami.

Wenye magari msiogope kwenda Mbagala mambo yameanza kubadilika. Nafikiri barabara hii inaweza kuwa moja ya barabara za kisasa nchini. Karibuni Mbagala!

No comments: