Saturday, January 24, 2009

Tuwaelimishe wauzaji wa vyakula kwa afya ya mlaji

Siku hizi watu wengi wanafanya biashara ndogondogo ili kuweza kupata kipato cha kukabili maisha ya kila siku. Biashara nyingi zinazofanywa zinahusu vyakula vya aina mbalimbali iwe vilivyotayarishwa au kutoka shambani kama vile matunda.Tatizo ninaloshuhudia kila ninapotamani kununua vyakula hivyo ni mazingira yanamouzwa biashara hizo.

Sawa, utamkuta mwanamama/dada anauza samaki wa kukaanga lakini chombo alichowekea samaki hao na ukimwangalia yeye mwenyewe hali ya usafi inakatisha tamaa. Mtu anauza maembe, ndizi, machungwa. Lakini usafi hakuna. Bibi anachuuza korosho za kukaanga kando ya barabara vumbi kibao, nzi kibao, karatasi za kufungia chafu! Kweli inatukatisha tamaa sisi walaji ingawa tunatamani kula au kutafuna vyakula hivyo. Tunapoingia kwenye soko huria ni vizuri wauzaji wa vyakula na matunda wakaelimishwa kwa faida yao na faida ya walaji wajali afya zetu.

No comments: