Thursday, January 22, 2009

Halmashauri ya Wilaya imedhamiria kuleta mapinduzi ya Kilimo

Gazeti la Kulikoni la tarehe 8 Januari 2009 lilikuwa na habari ya Halmashauri ya wilaya ya Rorya mkoani Mara ilivyotoa baiskeli 80 zenye thamani ya milioni 7 kwa wakulima wawezeshaji wapatao 80 kwa juhudi za kuhamasisha sekta ya kilimo wilayani humo. Huu ni mfano mzuri wa kuigwa kwa Halmashauri nyingine.

Ikumbukwe kuwa asilimia zaidi ya 80 ya wananchi wetu wanategemea kilimo. Kilimo kikiboreshwa ni dhahiri kuwa maendeleo yatapatikana na hapo ndipo maisha bora kwa wananachi walio wengi yatakapoonekana. Halmashauri zisiwe na mtazamo wa kukukusanya kodi tu. Waweke mikakati ya kuongeza uzalishaji hasa katika kilimo ili waweze kupata mapato zaidi yatakayowezesha kusaidia miradi mingine ya maendeleo kama vile ya elimu, afya na miundo mbinu.

No comments: