Wednesday, January 14, 2009

Maji machafu kutoka KTM

Unaposafiri kwenda Mbagala pale Mtoni Kizinga mkono wa kushoto utaona kuna maji maji pamoja na majani yaliyoungua. Unapopandisha kidogo Mbagala Mission upande wa kushoto kuna kiwanda cha nguo maarufu -KTM. Kiwanda hiki humwaga maji yake machafu yanayotoka kiwandani kwenye mto Kizinga.

Hutakiwi kwenda maabara kubaini kuwa maji hayo yana sumu kwani kwa macho ya kawaida kabisa unaweza kuona kote ambako maji hayo yamepita mimea imenyauka kwa eneo kubwa. Hii ni uthibitisho kuwa maji haya yanasumu kali. Hata hivyo ni ajabu kuona kuwa baadhi ya watoto wanaoga kwenye maji hayo machafu. Hivi karibuni blog hii imeshuhudia watoto wengi wakipiga mbizi kwenye maji hayo hasa wakati mvua nyingi inaponyesha kiasi cha kuchanganyika na maji hayo na kufanya bwawa kubwa hapo Kizinga.

No comments: