Saturday, January 24, 2009

Wakulima wanapouza vocha za pembejeo

Ukiwauliza wakulima wa Tanzania kwanini wanashindwa kulima kwa tija. Moja ya sababu wanazozitoa ni pembejeo za kilimo kuwa aghali mno hasa mbolea.

Kwa kuona hilo serikali imeweka mpango wa kuwapatia ruzuku ya mbolea wakulima kwa kupitia vocha za pembejeo. Sasa tunapopata habari kuwa, kuna wakulima wanauza vocha tena kwa bei rahisi ili waweze kupata fedha za kununulia mahitaji mengi basi hao si wakulima. Kuna haja ya kuwatambua wakulima wetu pengine si asilimia 80 kama tunavyodhani.

No comments: