Monday, February 2, 2009

KILWA ROAD UPDATE 4!

Matengenezo ya barabara ya Kilwa ( Mto Mtongani-Mbagala R3) yanaendelea vizuri licha ya mvua zinazonyesha kwa sasa kiasi cha kupunguza kasi ya utengenezaji wa baraba hiyo. Juma la jana Blog hii imeshahudia uwekaji wa lami kwenye keepleft ya Kizuiani pamoja na uwekaji wa lami kutoka St.Anthony Sekondari hadi sabasaba.

Tatizo kubwa ni kwa madereva wenye haraka wasiopenda kufuata utaratibu na kusababisha msongamano usio wa lazima hasa nyakati za asubuhi na jioni. Vinginevyo barabara inasonga mbele nina matumaini makubwa kuwa ifikapo mwezi watatu (Machi) usafiri wa Mbagala utakuwa bomba n tayari tumeshaanza kuyaona mabus mazuri yakija Mbagala!

No comments: