Tuesday, February 3, 2009

Biashara ya mchanga kati kati ya barabara!

Kuna mambo mengine yanaendeshwa hapa nchini kama vile hakuna usimamizi, hakuna sheria wala utaratibu wowote.

Wakati huu ambao barabara ya Kilwa inakarabatiwa kuwa ya kisasa zaidi ni ajabu kuona pale Mbagala Zakhem magari makubwa ya kusomba mchanga yakifanya biashara katikati ya barabara. Hivi kweli huu ni utaratibu uliopangwa na Halmashauri ya Manispaa ya Temeke? Hivi kweli viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke kuanzia madiwani, wabunge na wale wa serikali za mitaa hawajayaona magari haya? Magari haya ni moja ya kero ya usafiri kwa wakazi wa Mbagala. Hivi kwenye vikao vya madiwani huwa kinazungumzwa nini? Biashara hii ikome.

No comments: