Monday, February 2, 2009

NAMI NALIA NA PINDA

Kauli aliyoitoa Pinda kuhusu mauaji ya kinyama wanaofanyiwa ndugu zetu Albino ni kauli ya uchungu ni kauli inayoonyesha kuwa Serikali haitowavumilia wauaji hao wanapokutwa wakifanya tendo hilo. Hakuwa na maana kuwa mtu akituhumiwa auawe. Lakini akithibitika bila kuhoji basi nao wanastahili adhabu "kama hiyo."

Hivi sisi Watanzania tukoje? Mtu anaua, mtu anawakosesha raha watu wenzake halafu mnasema sheria sheria! Ah bwana kwa hili mimi nalia na Pinda wauwawe tu basi. Labda hayajakufika. Baba yako anauawa kinyama, mtoto wako, mke wako mama yako dada yako. Halafu wengine wanaleta siasa. Mimi nikumkuta nachinja!

Waziri Mkuu alilia kwa kuwa anajua ukubwa wa tatizo hilo. Tulie pamoja na Pinda

No comments: