Wednesday, February 4, 2009

Wanajipima wenyewe na kujiondoa mapema

Huwa sipendi kuwasifia Wamarekani kwa kila kitu, ila kwa hili la kujiondoa mapema wanapojiona kuwa wadhifa wanaopewa unaweza kuwaletea matatizo hapo baadaye Wamarekani wamefanikiwa sana.

Hivi Karibuni Rais Barack Obama aliwateua baadhi ya Wamerikani kushika ngazi za juu katika utawala wake akiwemo Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Huduma za Jamii Bw. Tom Doschel ambaye alijiondoa baada ya kuona kuwa alishindwa kulipa kodi ya kiasi cha $ 130,000. Hapa kwetu isingewekana. Kwa hili, Wamerekani nawapa shavu.

No comments: