Thursday, February 26, 2009

Temeke itengeneza barabara ya Kilungule

Wakati mwingine huwa najiuliza kuwa hivi kweli sisi tu wabunifu? Hata kidogo. Mi siamini kama kweli sisi ni wabunifu. Hebu fikiria mwenyewe, Madiwani wa Manispaa ya Temeke, Mkurugenzi na Meya wameshindwa kuweka mikakati ya kuifanya barabara ya Kilungule inayoungana na Yombo hadi Tandika - Davis Corner iweze kupitika wakati wote. Barabara hii ingekamilika ingepunguza kwa kiasi kikubwa matatizo ya usafiri kwa watu wa maeneo ya Mbagala. Juzi nilipita barabara hiyo ni fupi ajabu. Ni dakika 15 kutoka Charambe hadi TAZARA!

No comments: