Thursday, February 26, 2009

Watoto wetu kukosa madawati tulaumiwe wazazi

Nasikitika sana kusoma taarifa kuwa hadi hivi sasa wanafunzi wengi wa shule za msingi na sekondari hawana madawati ya kusomea. Kweli madawati ni ghali lakini tukijiwekea mikakati tunaweza kuwa na madawati kwa watoto wetu. Dawati ni hitaji muhimu kwa mwanafunzi. Hivi Wazazi tunashindwa kuchangia dawati moja kwa watoto wawili kwa miaka saba, au minne? Hata haiwezekani tuanze kuwapatia watoto wetu madawati. Tusingoje maagizo kutoka kwa waziri Mkuu.

No comments: