Tuesday, February 17, 2009

Wazaramo hawaachi kucheza ngoma

Baadhi ya Wazaramo wameendelea kudumisha utamaduni wao wa kucheza ngoma kwa muda mrefu. Juma lililopita, blog hii ilishuhudia ngoma iliyochezwa kwa muda wa siku 4 pale kijijini Kisemvule, Mkuranga mkoa wa Pwani. Siku ya Alhamisi shughuli ilianza kwa ngoma ya gombesugu na kumalizia rusha roho ya nguvu siku ya Jumapili. Si sare hizo, si mipasho hiyo, wageni kutoka Dar, mashindano ya kutunzana ndo usiseme. Hao ndiyo Wazaramo hawaachi utamaduni wa kucheza ngoma za kushindana.

No comments: