Tuesday, February 3, 2009

Benki tatu Mbagala Rangi 3

Ndiyo, huduma ya benki kwa miaka ya hivi karibuni imeongezeka sana katika Manispaa ya Temeke. Pale Mbagala Benki zote tatu maarufu nchini hutoa huduma kwa wananchi wa maeneo ya Mbagala hata wilaya ya Mkuranga na Rufiji. Benki hizo Ni NMB, NBC na CRDB.

Huduma zinazotolewa na Benki hizo kwa ujumla zinaridhisha. Kabla ya kuanza kwa huduma hizo hapo Mbagala wananchi walio wengi walikuwa wanapata huduma hizo Temeke na mjini sasa mambo safi. Kwa mfano kwa Benki ya NBC mara nyingi ATM yake huwa haina foleni kubwa. Kutokana na hali hiyo uwekezaji katika maeneo ya Mbagala unakuwa kwa kasi ya ajabu.

No comments: