Thursday, February 26, 2009

Hongera Taifa Stars-Asante Mrisho Ngassa

Juhudi binafsi za mchezaji Mrisho Ngasa ndizo zimetuwezesha watanzania kujidai katika mashindano ya CHAN yanayoendelea huko Ivory Coast . Pamoja na ufupi wake kama mwana blog hii lakini aliruka na kufunga goli la kichwa katikati ya mabeki wa Ivory Coast. Ufupi hoja kwenye kandanda? Alijituma, aliyafanyia kazi maelekezo ya mwalimu na kweli yamelipa. Nakumbuka gazeti moja lilimnukuu kocha Maximo akimweleza Ngassa aache kucheza na jukwaa. Ngassa amezingatia hayo na sasa anafanya maajabu. Kwa bahati nzuri nimeweza kuangalia mechi zote mbili ambazo Stars imekwisha cheza.Kwa kweli Ngassa amekuwa si nyota tu wa Taifa Stars bali nyota wa mechi zote 2. Asante Mrisho Ngassa.

1 comment:

Belo said...

Ile mechi ya kwanza tulifungwa sababu ya woga wa mashindano
Hongera Stars