Thursday, October 9, 2008

Kubonyeza kengele ovyo ndani ya bus si ustaarabu

Kutokana na tatizo la usafiri hapa jijini Dar Es Salaam.Mjasiriamali mmoja, tena Mtanzania ameleta mabus mazuri licha ya kuwa ni mitumba ili kuweza kuboresha usafiri hapa jijini. Mabus haya ni ya kisasa na ni makubwa. Kila dirisha lina kengele inayotumiwa na abiria kumtaarifu dereva asimamishe bus iwapo anataka kuteremaka kituoni au kama kuna dharura.

Jambo la kushangaza, abiria wasio wastaarabu wanazitumia kengele hizo vibaya kwa kubonyeza kila wakati na hivyo kumfanya dereva kusimama wakati hakuna anayeshuka wala hakuna dharura yoyote. Ndiyo maana nasema kubonyeza kengele ovyo ndani ya bus si ustaarabu. Kutonana na hali hiyo sasa kengele hizo hazifanyi kazi (disconnected).

No comments: