Wednesday, October 8, 2008

Traffic chunguza mabus ya Mkuranga-Kigamboni

Jumamosi iliyopita wakati narudi nyumbani kwangu nilipitia Kigamboni nikidhani kuwa nitapata usafiri mzuri nikiogopa foleni ya barabara ya Kilwa wakati wa jioni.

Waswahili husema nimeruka mkojo nimekanyaga mavi! Pale Kigamboni stendi ya mabus ya kwenda Kongowe, Mjimwema na Kibada mabus yenye maandishi ya Mkuranga -Kigamboni yalikuwepo lakini yalikuwa yanakatisha mwisho Kibada au Mjimwema. Usafiri ulikuwa ni wa shida sanaTulipoteza karibu saa moja kabla hatujakubaliana na kulipa shilingi 1,000/= kwenda Kongowe!

Mabus haya ya Kigamboni-Mkuranga kwa kweli hayasafiri kwenye njia iliyopangiwa ni ujanja tu wakupata njia, Traffic angalieni hilo wananchi wanaumizwa hali ni mbaya.

No comments: