Wednesday, October 8, 2008

MASAKI SASA INAPENDEZA

Ni muda mrefu sijawahi kutembelea maeneo ya Masaki (Oysterbay). Ukiondoa Baharini na beach zake sikuwa na sababu ya kwenda huko. Lakini Jumapili iliyopita nilipata mwaliko wa ndugu yangu anayeishi huko kuhudhuria sherehe za watoto wake waliopata komunio. Kwa kweli Masaki imebadilika sana. Nyumba nzuri zimejengwa na zinaendelea kujengwa. Barabara zimekarabatiwa, mitaro ya maji machafu inajengwa.Maduka mazuri yamefunguliwa. Wale mbuzi waliokuwa wakila michongoma sasa hawapo tena! Kweli Masaki sasa inapendeza hakuna tofauti na Majuu au South!

No comments: