Wednesday, October 15, 2008

Bei ya nyama ni juu Dar


Kwa wakazi wengi wa jiji la Dar Es Salaam hasa wa kipato cha chini kula nyama ni anasa. Bei ya nyama ya kawaida kwa sasa ni zaidi ya Tshs 3800/= kwa kilo. Hivi kweli kuna vigezo sahihi vinavyofanya nyama ipande kwa kiasi hicho?


Inasemekana hali si mbaya sana kwenye soko la jumla. Lakini wauzaji wa rejareja ndiyo wanaopandisha bei kiholela. Kibaya zaidi vipimo vinavyotumiwa si sahihi. Walaji wanadhulumiwa sana. Sijui kama Uongozi wa Jiji unafahamu hili. Hali ni mbaya lishe ya wananchi inakosekana hasa proteini inayopatikana kwa kula nyama.

No comments: