Wednesday, October 15, 2008

Msimu wa maembe umeanza

Msimu wa maembe umeanza. Dalili nzuri zinaonyesha ukipanda boti pale Kivukoni. Embe ndogondogo zilizoiva vizuri zikiwa zimepakiwa kwenye matenga zinavushwa kwenda mjini kwa kuuzwa. Embe hizi ni nzuri.

Tanzania tumebahatika sana kwa kuwa na hali ya hewa inayoweza kustawisha mazao mbalimbali na kwa misimu tofauti kwa gharama nafuu. Kilimo hiki ni kizuri lakini si endelevu. Kwa mfano hakuna mikakati ya kuweza kumuinua mkulima katika uzalishaji wa matunda, mboga, korosho na nafaka. Mabenki yetu haioni kuwa wakulima wanakopeshaka na kwa vile tu wanataka fedha zao zilirudi kwa msimu mmoja. Hii haiwezekani kwenye kilimo. Mkulima lazima apewe muda mrefu ili aweze kuzalisha kwa faida na kuweza kurejesha mikopo hiyo. Hali ni ile ile kila mwaka na mkulima ni yule yule, mfanyabiashara naye habadiliki kila mwaka kusukuma tenga la maembe machache kuyachuuza mitaani!

No comments: