Thursday, October 23, 2008

Machungwa bado yanapatikana Dar

Msimu wa maembe umeanza, lakini machungwa bado yanapatikana Dar tena kwa bei nafuu sana. Shilingi 100/= kwa chungwa moja. Machungwa ya sasa ni matamu sana. Nawapongeza sana wakulima wetu kwa jitahada zao kubwa za kuhakikisha kuwa karibu kila zao linapatikana mwaka mzima. Miaka ya nyuma ilikuwa ni nadra sana kula chungwa hapa Dar kwa wakati huu. Hii ni dalili nzuri kuwa kuna teknolojia imeongezeka katika kilimo. Hii ni dalili nzuri pia kuwa wakulima hawa wakiongezewa uwezo wanaweza kufanya makubwa.


Nchi yetu imebahatika kuwa agroekolojia mbalimbali ambazo zinaweza kustawisha mazao mbalimbali kwa nyakati tofauti. Vile vile zina aina tofauti za udongo licha ya kuwa na vyanzo vingi vya maji ambavyo bado havijatumika kikamilifu kwa uzalishaji wa kilimo.

No comments: