Wednesday, October 8, 2008

Dar ikitekeleza mipango yake itaipita Gaborone

Jiji la Gaborone ni dogo ukilinganisha na jiji la Dar Es Salaam. Wakazi wake pia ni wachache sana. Hakuna pilikapilika nyingi mchana na usiku. Maduka yake si mengi na wala si ya kutisha, lakini mipango ya kuendeleza jiji hilo ipo, inaonekana na inatekelezwa. Mji ni msafi, nyumba zimejengwa kwa mpangilio mzuri. Utaratibu wa usafiri umepangwa vizuri. Si rahisi kuona malori makubwa kwenye njia za magari ya abiria.


Dar Es Salaam tuna mambo mazuri mengi tu. Jiji kubwa, watu wengi, wajanja, wakarimu . Maduka mengi, bidhaaa mbalimbali na mazao mablimbali yanayopatikana wakati wote. Bahari tunayo, mvua inapatikana misimu miwili. Wasomi wapo, mipango mizuri ipo. Tatizo ni nini?


Hatutekelezi kikamilifu tuliyojipangia- Hilo ndilo tatizo kubwa! Blaa blaa nyingi tu. Mtu anakojoa mchana kweupe, hakuna anayejali! Malori yenye shenena za mafuta yanaachiwa bandarini saa 9.00 wakati wafanyakazi wanarudi kutoka kazini - matokeo take foleni yakujitakia kabisa! Hakuna anayejali. Hilo ndilo tatizo la Dar.Vinginevyo, naipenda Dar yangu na iwapo tutarekebisha mambo yetu, ukiondoa J'BURG, na Capetown miji mingine iliyobakia kusini mwa Afrika itaburuzwa na Dar.

No comments: