Wednesday, September 24, 2008

Kweli Botswana ni nchi ya nyama

Unapoingia kwenye ndege ya Air Botswana haipiti hata dakika 10 kabla hujarushiwa kipaketi cha nyama ya kukausha safi kilichofungwa vizuri utafune kwa raha zako huku wakikuuliza ni kinywaji gani unataka ushushie. Botswana hapo wanaanza kutangaza nyama. Jana jioni kwenye chakula cha jioni pale Grand Palm Hotel kulikuwa na nyama zilizotayarishwa kwa njia tofauti na ni nyingi tu. Mchana huu tumepata chakula chetu huku nyama zikiwa nyingi tu tena zimeandaliwa vizuri hata mifupa imekatwa vizuri! Ilibidi nimuulize Mtswana mmoja . "Nyie mnakula nyama sana hampati ugonjwa wa "gaoti"? Yeye alisema tatizo hilo limeanza kujitokeza sasa hasa kwa wanaokunywa pombe! Tanzania tunashindwa hata kuwatayarisha vizuri dagaa kamba "prawns" na kufanya bite kwenye AIR Tanzania?

No comments: