Wednesday, September 17, 2008

HIVI TUNAELEWA NYIMBO ZINAZOIMBWA KWA LUGHA YA KIINGEREZA?

Adamu Lusekelo ni Mwandishi Mwandamizi hapa nchini. Mimi binafsi ninamfahamu. Jinsi anavyoandika ndivyo alivyo. Soma Mraba wake wa LIGHTTOUCH kila Jumapili kwenye gazeti la "Sunday News" utapata ujumbe kama utamwelewa unachokiandika. Anaandika kwa lugha nyepesi na ya kuvutia yenye mzaha lakini..... Hiyo ndiyo maana ya LIGHTTOUCH - pengine niseme ni "kuuma na kupuliza." Jumapili hii alikuja na kichwa cha habari " The Nasty generation gap!" (MPASUKO KWA VIZAZI ---tafsiri yangu). Alipoandika kuwa vijana walikuwa wanafurahia nyimbo iliyokuwa ikiimbwa ya " Do me ! Do me !" huku wakiirudia rudia. Nabaki nikijiuliza, je vijana hawa wanajua maana ya nyimbo zinazoimbwa kwa kiingereza? Maana wasanii huwa hawaimbi kwa lugha Nyepesi. Wastafsiri "Do me" kwa tafsiri nyepesi. Kwa kawaida wasanii hutumia lugha za mafumbo. Msikilize Juma Nature, Ali Kiba, Nyoshi El Sadat, Muhidin Gurumo. Utafahamu nini ninachozungumza. Nyimbo hiyo kwa tafsiri sahihi ni MATUSI! Niwaambieni.

No comments: