Wednesday, January 23, 2008

TABORA MJI MSAFI

Mwezi Desemba mwaka jana (2007) nilikuwa mjini Tabora. Mimi si mgeni sana wa mji wa Tabora, nimeshatembelea Tabora karibu mara tano sasa. Lakini mwaka jana nilifurahishwa na hali ya usafi wa mitaa ya mjii wa Tabora.

Barabara zimefagiliwa, mitaro imezibuliwa na ni nadra sana kukuta lundo la taka kando ya barabara.

Nilipowauliza wenyeji, siri ya usafi wa mji wa Tabora, wengi walisema kuwa ,shughuli ya usafi katika mji huo ni shirikishi. Unaanzia kwenye kaya. Kila mwana kaya anawajibika, viongozi wa mtaa wanawajibika na Halmashauri nayo inawajibika. "Siku nyingine uchafu unazolewa mara mbili kwa siku."Anasema mkazi mmoja wa mji wa Tabora.

Si kwamba Tabora wana magari mengi ya kusomba uchafu. Kwanza sikuyaona magari hayo. Lakini wamejipanga.

Mjini Tabora huwezi kuona vibanda vya ovyo ovyo. Shughuli za biashara ziko sehemu zilizopangwa. Hata pale sokoni Tabora kuna mpangilio kuna sehemu za biashara ya kuku na nyingine za "Music Systems, TV, n.k."

Iiiiii kwa usafi mmewashinda watani zenu wa Morogoro. Mmewakandamiza kabisa! Tujage mwanawane. Manispaa Morogoro tumeni ujumbe Tabora mkajifunze usafi kidogo.

Lakini nimedokezwa kuwa Musoma ni kiboko ya usafi. Nitafika huko siku moja na "nitawakandamizia" ya huko kwenye blog hii.

Napendekeza uwepo ushindani wa usafi kwa miji yetu. Na washindi wapewe zawadi za kuiweka miji hiyo katika hali nadhifu.

Ni waulize swali.

"Ni kweli hatuwezi kutengeza ndege, usafi je?"

No comments: