Wednesday, January 23, 2008

Johnson Mbwambo ulichoandika ni sahihi

Moja ya makala yangu ya hivi karibuni katika blog hii ilikuwa ni kulikaribisha gazeti la Rai Mwema nikasema karibu mgeni wetu.

Mgeni huyu kwa kweli anafanya mambo mengi. Anafagia nyumba, anaosha vyombo baada ya kula chakula wakati mwingine anakwenda shamba na kubeba mizigo! Kweli mgeni njoo mwenyeji apone!

Moja ya toleo la Raia Mwema, mwandishi wake mahili Bw. Johnson Mbwambo aliandika kuhusu uamuzi wa kujenga kiwanda cha Magadi kwenye eneo la ziwa Natron. Mbwambo ameandika mengi kuhusu hasara itakayopatikana kimazingira kwa uamuzi huo hasa kusumbua viumbe hai (Ndege na wanyama) waliopo kwenye maeneo hayo. Aliwataja ndege aina ya Flamingo ambao ni adimu hapa duniani na wanapatikana kwa wingi hapa Tanzania. Watalii wengi huja kuwaona ndege hao na kwa kufanya hivyo huongeza pato la taifa.

Pamoja na athari nyingine nyingi kimazingira lakini wakubwa wameshakilia uamuzi wao wa kujenga kiwanda hicho ambacho inaonekana hakitakuwa endelevu wao wameshikilia kuwa kitatoa ajira kwa wingi. Sawa, lakini je ajira hizo ni endelevu? Au ndo mtu kishachukuwa chake kabisa?

Johnson ameandika, sisi tumekusoma. Raia Mwema atakuwa shahidi. Tusubiri tuone!

No comments: