Monday, January 14, 2008

WENGI HAWAIFAHAMU ASDP

Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo iliyozinduliwa mwaka wa fedha 2006/07 inatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa katika Sekta ya Kilimo.

Kwa kweli hata serikali ya awamu ya NNE chini ya uongozi wa Mh.Rais Jakaya Kikwete inaitegmea Programu hii kuboresha maisha ya wakulima wetu huko vijijini. Pamoja na matumaini makubwa waliyonayo hasa viongozi wa ngazi za juu, napenda kutoa maoni yangu kuwa wananchi wengi bado hawafahamu utekelezaji wa programu hii. Hii inathibitishwa na jinsi fedha zilizotumwa kwenye Halmashauri nyingi zinapokosa kazi.

Nilikuwa na mazungumzo yasiyo rasmi na mmoja wa wakuu wa wilaya hapa nchini. Alinieleza bila kuficha kuwa hata yeye hafahamu vizuri. Tatizo ni kwamba utendaji katika ngazi ya Halmashauri hauko wazi kwenye utekelezaji wa Programu hii ambako asilimia 75 ya fedha za programu hii hutumwa huko.

Kama hali ndiyo hii. Kwa kweli tuna kazi ya kufanya, ni lazima tupitie programu hii kwa haraka sana na tubadilike katika utendaji wa kutekeleza programu hii. Nina wasiwasi muda uliopangwa wa utekelezaji wa programu utapita na matokeo yasiwe mazuri. Hii ni lugha rahisi sana. Lakini ni hatari kwa maendeleo ya sekta hii.Tutambue hilo na ndo ukweli wenyewe.

No comments: