Friday, January 25, 2008

TABIA YA KUTELEKEZA

Nimevutiwa sana na picha ya lori lililotekelezwa huko Kantalamba Sec.School. Picha hiyo inaonekana kwenye blog ya Mjengwa.

Ndiyo, ugonjwa wa kutelekeza ni mkubwa sana kwenye jamii yetu. Umekuzwa hadi kwenye taasisi zetu za serikali ambako umeota mizizi. Gari jipya linaweza kutelekezwa kwa kukosa kipuri cha Tshs 20,000/=, kompyuta ya miezi 2 inaweza kutlekezwa kwa kukosa cartridge, pikipiki kwa kukosa tairi n.k.n.k. Eti taasisi imekosa fedha hizo.

Maggid, kuna vingi vimetelekezwa kwenye taasisi zetu na kama itafanyika "study" basi mioyo yetu itasimama jinsi raslimali zetu zinavyotelekezwa.

No comments: