Wednesday, January 23, 2008

JIJI LA DAR BADO CHAFU!

Mwaka mpya wa 2008 ndo umeshaanza na siku 22 zimeshakatika. Lakini Dar bado chafu! Dar bado ni ile ile ya mwaka 2007. Nimetembelea Kinondoni-chafu, Ilala- chafu na Temeke - chafu!

Mitaro imeziba, malundo ya taka yamezagaa barabarani. Nzi wanaruka ruka kwenye mabaa, migahawa na mitaani.

Dar unaweza ukajibanza pembezoni mwa barabara na kukojoa bila woga. Akukamate nani ? Huo ndo ustaarabu wetu na mgambo wa jiji akifanya hivyo anaambiwa noma mshikaji.

Siyo kusema kuwa sheria hakuna la hasha, zipo (Nitauliza viongozi wa jiji adhabu ya kukojoa ovyo jijini) ila utekelezaji wake ni wakishikaji. Mgambo wa "jiji" anaweza kukamata lakini ukimwachia shilingi 200 anakuachia, huku ukiwa umeacha uchafu na pengine ugonjwa! Tunauza ugonjwa kwa shilingi 200!

Tabia hii ya uchafu ipo ndani ya jamii zetu, nyumba zetu na ofisi zetu na wala hatujali. Hatuna maadili mema ya usafi. Hatutaki kuwafundisha watoto wetu usafi. Kwamba kutupa taka ovyo ni uchafu na ni tabia mbaya. Hatufanyi hivyo.

Kweli inatupasa kujipanga upya JIJI LETU KUBWA LA DAR BADO NI CHAFU!

No comments: