Friday, November 23, 2007

VETA MTWARA BORESHENI HUDUMA!

VETA MTWARA ni moja vyuo bora hapa nchini vinavyotoa elimu ya Ufundi. Chuo hiki kimejengwa kwa kufadhiliwa na serikali ya Japan. Chuo kimejengwa kando kando ya bahari ya Hindi sehemu inayojulikana Shangani ambayo ni maarufu sana pale Mtwara.

Chuo hiki kinauwezo wa kuchukua wanafunzi wapatao 1000 kwa wakati mmoja.
VETA Mtwara pamoja na kutoa mafunzo mbalimbali pia ina vitega uchumi vingi kama huduma za malazi, chakula na kumbi za mikutano.

Pamoja na mazingira mazuri yaliyopo VETA Mtwara, huduma zitolewazo bado ni hafifu hasa kwa upande wa chakula. Wahudumu hawachangamkii wateja na unapotaka huduma unaweza kuambiwa hakuna. Chakula- Hakuna, Kinywaji - Hakuna. Eh basi kwaheri.

Kwa kweli inasikitisha wakati mwenyeji wako anapokutoa na kukupeleka mahali fulani ambapo anategemea kuwa unaweza kupata huduma safi anavunjwa moyo na hizi HAKUNA HAKUNA.

VETA Mtwara ni Taasisi ya kujivunia mjini Mtwara na sitoshangaa kama itakuwa CHUO KIKUU hapo baadaye. Lakini boresheni huduma zenu.

No comments: