Tuesday, September 11, 2007

HAMKUJUA KAMA NI MHINDI?

Mengi yamesemwa kuhusu Mshindi wa Miss Tanzania wa mwaka huu. Wengine wanalalamika eti kwanini mshindi amekuwa Mhindi? Jamani, huyu Mhindi ametokea mbali katika Kinyanga'anyiro hiki nafikiri kutoka Mtaa hadi pale wilayani Kinondoni. Wakati anashinda pale Kinondoni hakuwa Mhindi? Je, Richa Aidha alipokuwa Miss Earth 2000 kule Phillipines hakuwa mhindi? Miss Indian Ocean 2006 hakuwa mhindi ?Watanzania acheni ubabaishaji.

Mimi siyo mfuatiliaji mzuri wa mashindano haya kwani nayaona ni ya kibabaishaji. Tunaigaiga tu mamabo bila kufahamu jinsi yanavyoendeshwa. Ndo maana akipatikana mshindi Mhindi tunaanza kulalamika lakini huko tunakokwenda tunawata wahindi, waingereza, warusi, wajapani sasa cha ajabu kipi. Vigezo vilivyowekwa ni vya kimataifa. Si vya Kiluguru (kucheza ngoma), Kichagga (kukatiakatia majani ng'ombe) kizaramo (shughuli)................

Kama uwezo wa Richa wa kuongea Kiingereza ni mkubwa kuliko wengine kwanini wengine wasiongea lugha wanayoifahamu vizuri (kiswahili). Sote tunafahamu tulio wengi uwezo wetu wa kuongea kiingereza ni ule wa ehe eh! You know, the, the nyingi tu. Mtu anaambiwa chagua utaongea kwa kutumia lugha gani anasema "English" haya mama twende kazini. Hata kueleza jinsi anavyoifahamu Tanzania hoi! Sasa tunalalamika nini? We Hoyce Temu mwaka 1999 ulikuwa Miss Tanzania kwenye mashindano ya Miss world hukuiona hata namba 50! Hakuna siasa hapa tupeleke wawakilishi wenye vigezo vinavyokubalika. Tikitaka dada zetu weusi washinde tuwaandee vizuri kwani huko wanakokwenda weupe ni wengi kuliko WEUSI. Hongera Richa usijali maneno ya Waswahili ndo walivyo.

No comments: