Monday, July 13, 2015

Hii ni familia yangu


Ndiyo. Hii yote ni familia yangu. Ni siku mtoto wetu Frt. Linto alipokuja kutuaga pale nyumbani Kisemvule. Frt. Linto anatoka India, lakini kwa takribani mwaka mmoja alikuwa parokiani kwetu Vikindu  kwa uchungaji. Alipopewa vazi la kuwa Frateri yeye alituomba mimi na mke wangu (Nancy) kuwakilisha wazazi wake ambao wasingeweza kuwepo siku hiyo. Kwa hiyo Linto ni mmoja wa familia yangu. Kwa sasa Ftr. Linto yuko Uganda kwa muda baadaye ataelekea Nairobi kwa masomo ya Teolojia.Pichani pia wanaonekana  waseminari ambao walikuwepo kwa mwaka mmoja parokiani kwetu wakianza mafunzo ya useminari kwa sasa wako Uganda.

No comments: