Monday, July 13, 2015

Africana Group kwa Christian Mkoba




Africana Group ni kundi la familia linaloundwa na ukoo wa Wambiki na watoto wao kwa asilimia kubwa. Kundi hili lipo jijini Dar Es Salaam. Lengo Kuu la kundi hili ni kudumisha uhusiano wa kifamilia uliokuwepo tangu zamani kwa bibi na babu zetu ambao makazi yao ni Morogoro, Matombo, Nige-Kariakoo. Kila mwezi hukutana mara moja nyumbani kwa mwanakikundi. Mwezi Juni Africana Group ilikutana nyumbani kwa ndugu yao Bw. Christian Paul Mkoba huko Kisemvule,wilayani Mkuranga, Pwani. Wakati mkutano unaendelea wajumbe wanaendelea na chakula pamoja na vinywaji walivyoandaliwa na mwenyeji wao.

No comments: